Je kunamadhara yoyote iwapo hutashiriki tendo la ndoa kwa muda mrefu?
Katika maisha ya kila siku ni jambo la kawaida kwa
mtu yeyote ambaye ameshafikia umri wa balehe kufikiria au hata kushiriki tendo
la ndoa. Katika jamii nyingi, kushiriki tendo hili imehalalishwa kwa ajili ya
wanandoa pekee na hujulikana kama tendo la ndoa. Tendo hili pia hufanywa kwa
ajili ya kujiburudisha kama starehe, kwa watu wa umri tofauti tofauti na
hujulikana pia kama kufanya mapenzi. Lakini, Je kuna madhara yoyote kama mtu
hatashiriki tendo la ndoa kwa muda mrefu?
Kiwango cha kushiriki tendo la ndoa hutofautiana
kati ya mtu na mtu na pia hutofautiana kulingana na umri. Hakuna kiwango
maalumu ambacho kinatambulika kuwa ni kiwango sahihi cha kushiriki tendo la
ndoa au mara ngapi inatakiiwa mtu ashiriki kwa wiki au kwa siku. Tafiti zinabainisha
kwamba, iwapo mtu hatashiriki mapenzi kwa miezi kadhaa au miaka, ananafasi
kubwa ya kutokuona mabadiliko yoyote mabaya kiafya.
![]() |
Photo by ROMAN ODINTSOV from Pexels |
Tafiti pia zinabainisha kwamba kushiriki mapenzi
mara kwa mara kuna faida kiafya kama vile kuimarisha kinga ya mwili, kupunguza
shinikizo laa juu la damu, kupunguza mfadhaiko, na kupunguza hatari za kupata
magonjwa ya moyo.
Baadhi ya faida hizi kama vile kupunguza mfadhaiko
huweza kupatikana kwa kujichua (masturbation).
Kwa wanaaume, afya ya tezi huimarika kwa kuejaculate
mara kwa mara. Utafiti uliofanyika mwaka 2016 uligundua kwamba kwa wanaume
ambao hu ejaculate angalau mara 21 kwa mwezi wananafasi chache sana kupata
saratani ya tezi kulinganisha na wale ambao wana ejaculate mara 4-7 kwa mwezi.
Utafiti huu ulifanywa na Jennifer R. Rider, Kathryn M. Wilson na washirika,
ulichapishwa tarehe 28 March 2016 katika jarida linalojulikana kama The Journal
of European Eurology.
Kwa wanawake, kushiriki mapenzi mara kwa mara
kuimarisha misuli ya nyonga ambayo hushikiria kibofu, kuimarisha kazi ya kibofu
na kupunguza athari za kushindwa kuzuia mkojo (urinary incontinence and
leakage)
Je kuna faida zozote za kufanya mapenzi/tendo la ndoa?
Kufanya mapenzi kuna faida kadhaa kwa afya ya mwili
na akili. Hizi ni baadhi ya ffaaida za kufanya mapenzi
·
Kupunguza stress/mfadhaiko: Kufanya
mapenzi husababisha mwili kutoa homoni kama vile oxytocin na endorphins, ambayo
husaidia kupunguza mfadhaiko na kuboresha ustawi wa kihisia.
·
Kupunguza hatari ya magonjwa ya moyo:
Kufanya mapenzi kuna faida za kiafya kama vile kupunguza shinikizo la damu na
kuboresha mtiririko wa damu, jambo ambalo linaweza kupunguza hatari ya kupata
shinikizo la juu la damu.
·
Kupunguza maumivu: Kufaanya mapenzi
husaidia kuuachiliaa homoni za kuzuia maumivu kama vile endorphins, ambazo
hupunguza maaumivu na kufanya ujihhisi vizuri.
·
Kuboresha usingizi: Kufanya mapenzi
husaidia kupunguza mkusanyiko wa homoni za mfadhaiko mwilini na hivyo kukufanya
kupata usingizi bora.
·
Kuimarisha kinga ya mwili: Kufanya
mapenzi husaidia kuimarisha kinga ya mwili kwa kusababishaa kuzalishwa kwa
kemikali ambazo husaidia kuondoa dalili zitokanazo na maambuziki ya vimelewa
wasababishao magonjwa hasa virusi.
·
Kuboresha afya ya akili: Kufanya mapenzi
husaidia kuondoa dalili za unyongovu, kupunguza wasiwasi na kuboresha hisia za
furaha.
Kufanya maapenzi inatakiwa kuwa kwa hiari na kwa
usalama ili kuffurahia faida hizi.
Athari za kutofanya mapenzi
Ni kawaida kwa watu kukosa tendo la ndoa kwa muda
mrefu kutokana na sababu mbalimbali kama vile kuwa mbali na mwenzi wako, kukosa
maelewano katika mahusiano, matatizo ya kiafya au sababu nyinginezo. Hata hivyo
hali ya kukosa tendo la ndoa kwa muda mrefu inaweza kuathiri afya ya akili.
·
Mfadhaiko: Kutofanya mapenzi kunaweza
kusababisha mkusanyiko wa homoni za mfadhaiko. Hali hii huweza kupelekea kuwa
na wasiwasi, kukosa ujasiri wa kufaanya tendo la ndoa kwa ufanisi na mfadhaiko
·
Kukosa usingizi: Kufanya mapenzi
kunaweza kusaidia kupunguza mkusanyiko wa homoni zza mfadhaiko mwilini na
kusaidia kupata usingizi bora. Kukosa usingizi kunaweza kusababisha uchovu na
kusababisha matatizo ya afya ya akili na mwili.
·
Kuongezeka kwa hatari yaa magonjwa:
Kufanya mapenzi kunaweza kusaidia kuimarisha kinga ya mwili. Kutofanya mapenzi
kunaweza kuongeza hatari ya kuugua magonjwa kama vile shinikizo la damu,
magonjwa ya akili, na magonjwa ya mfumo wa kinga ya mwili.
·
Kuongezeka kwa hatari ya kiharusi:
Kufanya mapenzi kunaweza kusaidia kupunguza shinikizo la damu na kuboresha
mtiririko wa damu. Kutofanya mapenzi kuunaweza kuongeza hatari ya kiharusi
·
Kupungua kwa hamu ya kufanya mapenzi; Kama mtu
hajafanya mapenzi kwa muda mrefu anaweza kupoteza hamu ya kufanya mapenzi na
kuwa na uwezekano mkubwa wa kutohitaji tena tendo la ndoa. Hii inaweza kuathiri
maisha ya mahusiano na mwenzi wako.
·
Msongo wa mawazo: Kutokana na kushindwa
kutekeleza haja ya kijinsia, mtu anaweza kukumbwa na msongo wa mawazo na
huzuni.
·
Matatizo ya kiafya: Kutokana na kukosa
tendo la ndoa kwa muda mrefu, mtu anaweza kuwa na hatari ya kupata matatizo yaa
kiafya kama vile matatizo ya kushindwa kusimamisha uume (erectile dysfunction)
au matatizo ya kizazi kwa wanawake.
0 Comments